Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (kulia) akikagua Mitamba inayozalishwa katika shamba la kuzalishia mifugo la Mabuki wakati wa Ziara yake Januari 24, 2026 Mabuki, Mkoani Mwanza.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (Wa kwanza, kushoto) akizungumza Ujumbe wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) nchini Tanzania kujadili miradi inayotekelezwa katika sekta ya mifugo na uvuvi, wakati wa Kikao kilichofanyika ofisini kwake Januari 16, 2026 Mtumba, Jijini Dodoma.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa akiwalisha chakula samaki kwenye moja ya mabwawa yaliyopo kwenye kituo cha ukuzaji Viumbe Maji cha Rubambagwe kilichopo Chato mkoani Geita Januari 05,2026.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa akimwagilia malisho ya Mifugo mara baada ya kufika kwenye shamba darasa la Mifugo la Bw. Shakiru Kyetema lililopo Muleba mkoani Kagera Januari 02,2026.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (katikati) akiwalisha samaki chakula kwenye eneo la Lake Side mkoani Mara huku akishuhudiwa na baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Wizara yake na Ofisi ya Mkuu wa mkoa huo Desemba 22,2025.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa na Naibu wake Mhe. Ng’wasi Kamani wakivuna samaki kutoka kwenye moja ya vizimba vilivyopo kwenye ziwa Victoria eneo la Lake side mkoani Mara Desemba 22,2025.